Kama jana nilikuacha unaelea basi nakuomba radhi ila soma tena halafu uendelee na ya leo.
Leo naanza kwa kusema ni jana tuliongelea vitu vichache kuhusu maisha baada ya chuo kuingia mtaani.
Haijalishi umechelewaje kufanya mambo ila kama imepangwa utoboe lazima utatoboa.
Tuongee uhalisia kuna watu makundi mawili pindi chuo kinafunguliwa au masomo yeyote yanapoanza.
Kundi la kwanza na la pili ni kama yafuatayo.
ni wale wanaojua wanasoma nini na wanajua nini kinawapeleka shule, halafu kuna kundi la watu wanaenda shule kwa sababu ndiyo hatua (the next stage) wanayotakiwa kuchukua. Mimi kiukweli sijui ulikuwa stage gani ila hapa ndio hatua ya kwanza ya kuweza kujisaidia kuingia mtaani.
Sasa kama ulikuwa unajua unafanya nini shule au huelewi mimi sio jaji wa maisha ila kuna jambo la kuchunguza mara nyingi kwa sisi ambao hatujielewi ni presha tulionao kutoka kwa mazingira tuliotoka ikiwemo kama mzazi mlezi au ndugu haya yote yanaletwa kwa sababu zifuatazo ninazozielewa
Kwanza Mifumo yao wanataka iwe yetu:
Kila mtoto au kila mtu ana mfumo wake wa malezi ukiangalia familia zenye mtoto zaidi ya mmoja ukiangalia wazazi ni wale wale ila kila mtoto ana namna ya malezi. sasa hili watu wengi hawajui na tunaishia kuona kama kila jinsi mtu anavyoishi ndivyo na sisi tunabidi tuishi. Hapana. “haijalishi umechelewaje kufanya mambo ila kama imepangwa utoboe lazima utatoboa” usijifananishe namna yako ya maisha
na namna ya maisha ya mtu mwingine. Si laumu ila wazazi wengi wanataka watoto waunge tela. wawe pale nyuma yao wafanye vile vile walivyofanya wakiwa vijana. Kama alikuwa daktari atataka mtoto wake awe daktari kwa hyo inabidi mtoto afuate kila njia aliyopitia.
Ya Majirani Kwetu
Saa ingine mafanikio au maneno ya watu huleta adhari kwenye maamuzi ya walezi au hata wazazi wetu. Utasikia wewe fulani kuwa kama mtoto wa fulani unaona kaenda chuo kachukua engineering kawa mtu wa serikali, bila kujali hata mtoto anataka nini sasa haya huleta shida kwa mtoto bila hata mzazi kujua kwa haraka.
Madhara yake ni wazi kwa maisha ya watoto mfano ni ngumu kufanya maamuzi binafsi.
Embu mtafute mwanafunzi aliyemaliza chuo kwa ngazi ya diploma au degree kwa haraka haraka muulize nini kinafuata? wengi watakuambia hawajui na wengi wanaona njia rahisi ni kuendelea kusoma si semi kusoma si jambo zuri ila naona kama ni njia ya kukimbia ukweli. jana tuliona suala zima la deadlines as mtu yuko rahisi kuendelea
kusoma kisa ndo njia rahisi kwake kuwa na control ya mambo yake. Ukiwa shule unnaweza kuwa na usukani wa mambo kisa ni mambo machache tu unayofanya ambayo utawaza tu ada,modules na wapi utapata chakula, mavazi na wapi utalala. ila mtaani life haieleweki mambo yanakuwaga mengi kiasi wengi wanaogopa ingia mtaani kupambana
